November 30, 2015

Meli mpya ya Serikali ya Zanzibar Mv  Mapinduzi II inatarajiwa kufika Zanzibar  Disemba 2 mwaka huu baada ya kumalizika kwa matengenezo yake.
Meli hiyo imetengenezwa  Korea ya kusini kwa gharama ya dola za Kimarekeni milioni 30.6 ilitarajiwa kuwasili Zanzibar  mwezi Julai 2015 lakini imechelewa baada ya kuwekewa kuzuizi na kampuni moja ya Leomthong  ya Thailand.
Kampuni hiyo ilikuwa inaidai Shirika la Biashara za Nje Zanzibar BIZANJE lililokuwa likiingiza vyakula na bidhaa mbalimbali katika miaka ya 80.
Katibu Mkuu wizara ya Fedha Khamis Omar amesema kufuaitia zuia hilo walifungua kesi mahakani kwa kuwa madai hayo  hayakuwa na  sasa meli ya MV Mapinduzi II ipo njia baada ya kuanza safari ya kuja Zanzibar kutoka Mauritius tangu Novemba 26.
Meli hiyo inachukuwa nafasi ya meli ya mwanzo MV Mapinduzi iliyotengenezwa chini ya utawala wa  Rais Aboud Jumbe Mwinyi iliyouzwa mwaka 2011 na  ilizama katika bahari ya visiwa vya Sychelles ikiwa ikielekea nchini Yemen kwa ajili ya matengenezo mara baada ya kuuzwa.

0 comments:

Post a Comment