Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameongoza
mamia ya wananchi na viongozi katika maziko ya marehemu Mzee Hamid
Ameir muasisi wa mapinduzi.
Marehemu Mzee Ameir aliekuwa pia Mwenyekiti wa
baraza la wazee wa CCM ameezikwa leo kijijini kwao Donge wilaya ya kaskazini B.Unguja.
Alifariki jana katika hospitali ya Mnazi mmoja
alipokuwa amelazwa kwa matibabu.
Mungu amlaze mahala pema peponi AAMIN.
|
Waziri wa nchi Ofisi ya
Makamo wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Mohammed
akisoma risala ya na wasifu wa Marehemu Mzee Hamid Ameir
Muasisi wa
Mapinduzi, pia Mwenyekiti wa Baraza
la Wazee wa CCM baada ya kuzikwa
leo Kijijini kwao Donge wilaya ya Kaskazini
B.Unguja.
|
|
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
(katikati) pamoja na
Viongozi wengine na wananchi wakiitikia dua iliyoombwa
baada ya
kuzikwa Marehemu Mzee Hamid Ameir
Muasisi wa Mapinduzi,
pia Mwenyekiti wa Baraza
la Wazee wa CCM leo Kijijini kwao
Donge
wilaya ya Kaskazini B.Unguja.
|
0 comments:
Post a Comment