February 03, 2016

Zaidi ya shilingi milioni mia moja zimekusanywa na Idara ya Mazao ya baharini Zanzibar kufuatia kuuzwa kwa mazao ya baharini ne ya nchi katika kipindi cha mwaka jana 2015
Makusanyo hayo ni ongozeko la shilingi milioni 69 zilizokusanywa  katika mwaka 2014 kwa  bidhaa za mwani, dagaa, kamba, majongoo na kaa .
Mkurugenzi wa idara hiyo Mohamed Soud Mohamed amesema ongezeko hilo linatokana na mwamko wa wananchi kujishughulisha na uvuvi wa kibiashara kufuatia zingatia taaluma zinazotolewa katika kukabiliana na soko la usindani kimataifa.
Hata hivyo amesema kuna upungufu wa usafirishaji nje ya nchi pweza na ngisi  kutokana na kuimarika soko la ndani hasa kwa kukua kwa sekta ya utalii nchini.
Mkurugenzi Mohamed ameyataja mazao mengine ya baharini yanaongoza katika kuingiza fedha ni dagaa liokusanya shilingi millioni kumi na tisa na shillingi miilioni thamanini kwa zao la mwani.

 

0 comments:

Post a Comment