January 26, 2016



Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imetiliana saini hati ya makubalino na taaisi ya Good Neighbour Tanzania kwa ajili ya ujenzi wa skuli ya sekondari na kituo cha utangazaji wa redio na televisheni.
Skuli hiyo itakayokuwa na madarasa 12  itajengwa huko kwarara wilaya ya Magharibi B kwa ushirikiano kwa ushirikiano na taasisi mbalimbali za korea ikiwemo shirika la utangazaji la nchi hiyo SBC, kampuni ya uhandisi na Shirika la maendeleo la Korea KOICA litakalotoa zaidi ya shilingi bilioni 2.1 za kitanzania.
Akizungumza baada ya utiaji saini huo katibu mkuu wizara hiyo Khadija Bakari Juma amesema mradi huo utapunguza matatizo ya wanafunzi wa eneo hilo kufuata skuli masafa ya mbali hali itakayoondosha wasiwasi kwa wazazi.
“Kwa kweli hii ni faraja kubwa kwa wanafunzi  eneo hili la kwarara lilokosa skuli kwa muda mrefu wanaolazimika kuenda  hadi fuoni au maeneo mengine ya mbali ili kufuata masomo” amesema.
Katibu mkuu amelishikuru shirika hilo kwa kufanikisha  mradi huo utakaonza hivi karibuni na kituo chake pia utafanikisha kutumia kuandaa vipindi vya kutoa elimu kwa uhakika huku pia akiahidi wizara hiyo itaiisaidia kupata masamaha wa kodi wa vifaa mbalimbali itakavyotumiwa katika ujenzi huo.
Nae mwakilishi  mkaazi wa taasisi  ya Good Neighbor ya Tanzania Namun Heo amesema wataweka vifaa vyote vya utangazaji nadani ya studio ya skuli hiyo pamoja na kutoa mafunzo kwa watendaji nchini Korea na wengie watakuja Zanzibar kufundisha

Amesema pia ndani ya kituo hicho cha matangazo lengo ni kuandaa pia vipindi mbalimbali vya kutoa elimu kwa jamii ikiwemo haki za wanawake watoto na masuala mengine  muhimu katika maisha ya  kila siku.


0 comments:

Post a Comment