Jeshi la polisi Mkoa wa Kusini Unguja
limesema hoteli ya kitalii ya Konokono iliyopo Michanvi Mkoani humo imeungua kutokana na moto
uliokuwa ukiwashwa karibu na hoteli hiyo.
Hoteli hiyo iliyoungua jana majira ya saa
5:30 inamilikiwa kwa pamoja na Bi Amina Amani Abedi Karume na ria wawili wa Italia
Andrea Chiapo na Luca Gambilura ambapo nyumba tatu na mgahawa mmoja
iliungua na kusababisha hasara ya shilingi milioni mia nne.
Kamanda wa polisi Mkoa huo Juma Sadi Khamis
amewaambia waandishi wa habari kuwa upelezi umeonesha kuwa moto huo
uliwashwa na watu waliokuwa wakisafisha eneo la kiwanja karibu na hoteli
hiyo na cheche zake ziliruka kufuatia upepo mkali na kuleta madhara hayo.
“Mimi naona tusiwe tunakuza mambo sisi
tumegundua hivyo wala si kweli hoteli hiyo haijachomwa kwa sababu za kisiasa kama inavyodaiwa na baadhi
ya watu”. amefafanua Kamanda Sadi.
Ameongeza kuwa tayari watu wawili
waliokuwa wakisafisha eneo hilo wanaendelea kushikiliwa na jeshi hilo kwa
uchunguzi zaidi.
Kamanda Sadi amefahamisha kuwa si busara
watu kutoa taarifa bila ya uchunguzi kwani matukio ya kuungua moto kwa aina
hiyo katika kipindi cha kiangazi yanatokea mara kwa mara abapo hivi
karibuni hoteli nyengine ya Mnana iliyopo kizimkazi na nyumba moja iliungua
huko Dunga.
0 comments:
Post a Comment