March 03, 2016

Bodi ya Elimu Mkoa wa Kusini Pemba imesema tatizo la wanafunzi wa Mkoa huo kufanya vibaya katika mitihani ya Taifa iliyopita ya mwaka 2015 linachangiwa na uzembe wa  baadhi ya walimu, wanafunzi na wazee katika kusimimia maendelo ya masomo.
Imeongeza pia  uwezo mdogo wa walimu kufundisha, uhaba wa walimu wa fani mbali mbali hasa masomo ya Sayansi huku pia baadhi ya walimu wanaonekana hawana hamu ya kazi hiyo.
Bodi hiyo katika kikao chake chini ya Mwenyekiti wake Omar Khamis Ameir kilijadili matokeo ya mtihani wa kidato cha nne na kutoa wito kwa pande zote zinazohusika na maendeleo ya elimu katika Skuli mbali mbali zijitahidi kutekeleza wajibu wao ili matokeo yajao yawe mazuri.
Aidha wamependekeza kuangaliwa mfumo wa utoaji wa ajira za walimu ili kupata walimu bora wanaofanya kazi kwa umakini zaidi.
Wakati huo huo Bodi hiyo imeikagua Skuli ya Sekondari ya binafsi ya Farahedy iliopo Mkoroshoni iliyoomba usajili wa kudumu na kupendekeza kupatiwa usajili huo kutokana na kukidhi vigezo.

Msimamizi wa Skuli hiyo Sheikh Saleh Omar amesema tatizo la kukosa usajili wa kudumu limekuwa ni kikwazo kwa Skuli hiyo kupata wanafunzi wa kutosha na msaada kutoka sehemu mbali mbali.

0 comments:

Post a Comment