January 18, 2016

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imepiga marufuku kitendo cha baadhi ya skuli za sekondari kuawatoza wanafunzi michango ya fedha tofauti na kiwango kilichoruhusiwa na serikali.
Katibu mkuu wizara hiyo Khadija Bakari Juma amesema kumekuwa na malalamiko mengi ya wananchi  kuwa  baadhi ya skuli inawalazimiasha wanafunzi kuchangia kiwango kikubwa cha fedha  kinyume na tamko la serikali la mwaka 1999.
amefahamisha tamko hilo limelekeza viwango vya uchangiaji kwa mwanafunzi ni shilingi 5000 kwa   darasa la tisa na kumi,  kidato cha tatu na cha nne ni shilingi 7500 na kidato cha tano na sita wanatakiwa kulipa shilingi 10000 tu.
Akizungumza katika kikao cha walimu wakuu na watendaji wa Wizara ya elimu na mafunzo ya amali amewataka walimu kulisimamia tamko hilo kwa ajili ya maendeleo ya wanafunzi  kwani bado linaendelea kutumika.
Katibu Khadija ameomba walimu hao kuwajibika  katika   kazi zao na kuhakikisha wanamaliza mihutasari ya masomo na kuacha kuwafundisha wanafunzi kikamilifu ili kuongeza ufaulu.

Kwa upande wao  walimu  hao wakuu wameiomba wizara ya elimu kufanikisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia katika skuli  pamoja na kuharakisha uungwaji wa huduma za maji na umeme ili kupunguza viwango hivyo vya uchangiaji kwa wazazi.

0 comments:

Post a Comment