January 15, 2016



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ameteua  Chimbeni Kheri kuwa Mshauri wa Rais katika masuala ya utamaduni,  Juma Hassan Juma Reli ameteuliwa kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango ya Zanzibar na Mdungi Makame Mdungi  anakuwa Katibu wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi  Dk. Abdulhamid Yahya Mzee Rais  Shein pia amemteuwa  Kai Bashir Mbarouk kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria na Noah Said  kuwa Mkurugenzi wa uendeshaji na Utumishi katika Wizara ya Kilimo na Maliasili.

0 comments:

Post a Comment