January 29, 2016

JUMLA ya kesi 106 za makosa ya usalama barabani zimekamatwa kufuatia operesheni maalum iliyofanywa na Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Unguja.
Kesi hizo zimehusisha vyombo mbalimbali vinavyotumia barabara ikiwemo vespa, gari za abiria ambazo zimewekwa tinted uchakavu wa vyombo pamoja na kumalizika kwa bima na leseni za njia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Juma Saadi Khamis, amesema katika operesheni hiyo wameamua kuanza kutoa hukumu ya papo kwa papo kwa wanaokutwa na makosa ya aina hiyo.
Amfahamisha kuwa katika wiki  iliyopita jumla ya vyombo 75 walishitakiwa na jumla ya faini ya shilingi 2,526,000/= zilipatikana.
Amesema kuwa hivi sasa operesheni hizo za kikosi cha usalama barabarani ni endelevu ili kuzuwia makosa ya barabarani. Amewashauri madereva wanaoendesha vyombo vya moto kuwa waangalifu wanapokuwa barabarani, sambamba na kuvipasisha vyombo vyao ili kuweza kuepuka makosa yasiyokuwa ya lazima.
Hata hivyo Kamanda Saadi amesema kuwa malengo ya Mkoa huo ni kudhibiti ongezeko la makosa ya usalama barabarani na kupunguza ajali zisizokuwa za lazima, sambamba na kutoa elimu kwa wadau dhidi ya matumizi sahihi ya barabara.

Akizungumzia ulinzi wa mkoa wa Kusini kamanda Saadi amesema wameijipanga kuwadhibiti  wahalifu wakubwa na baadhi ya watu wanaojihusisha na uvunjifu wa amani  na  usalama kwa watu na mali zao mkoani humo.

0 comments:

Post a Comment