January 30, 2016

Jumla ya eka tisa  (9)  za mashamba ya mikarafuu imechomwa moto na watu wasiojulikana na kusababisha hasara kuwa kwa wamiliki ya mashamba hayo katika bonde la Mkanyageni Shehia ya Mzambarauni Wilaya ya Wete  Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Moto huo ulilotokea Janauri 22 mwaka huu umeathiri zaidi ya mikarafuu 151 katika mashamba hayo.
Akizungumza katika eneo la tukio Mkuu wa  Wilaya ya Wete  Rashid Khadidi Rashid amesema kitendo cha kuchoma moto mashamba hayo ni kuhujumu uchumi wa nchi pamoja na wananchi wake na serikali itahakikisha inawasaka na kuwakamata wahusika ili kufikishwa mahakamani .
Amefahamisha kuwa kuchomwa moto mashamba hayo ni hujuma za makusudi zilizofanyika , kwani moto huo umetokea katika  maeneo na mashamba tofauti.
“Serikali haiwezi kuvifumbia macho vitendo vya kuhujumu uchumi wake, hivyo naviomba vyombo vya sheria kufanya uchunguzi wa kina ili wahusika waweze kupatikana na kufikishwa mahakamani ”amesisitiza.
Mmoja wa wananchi wakaazi wa shehia hiyo  Hamad Bakari Makame  akizungumza na mwandishi  wa habari hizi amesema kitendo hicho kimesababisha athari kubwa ya kiuchumi na kimazingira .

Amefahamisha kuwa mkarafuu mmoja unauwezo wa kuzalisha zaidi ya pishi ishirini ambazo kwa sasa ni sawa na zaidi ya shilingi laki nne. 

0 comments:

Post a Comment