Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein amesema
kuwa miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM ni kilele tosha cha kupatikana kwa maendeleo
katika Nyanja mbali mbali za kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Amesema kuwa maendeleo yaliyopatikana katika serikali zote mbili
ya Tanzania bara na Zanzibar yamesimamiwa na miongozo, ilana na mikakati mbali
mbali iliyotokana na CCM.
Alikuwa akizungumza katika uziunduzi wa miaka 39 ya kuzaliwa kwa
chama hicho katika viwanja vya Afisi kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar,
Dkt. Shein amesema kuwa CCM iliyozaliwa mwaka 1977 baada ya
kuungana kwa vyama viwili vya ukombozi vikiwemo TANU na Afro shraz party (ASP),
chama hicho kimeweza kupigania haki za wanyonge kwa kusimasmisha serikali zenye
misingi imara ya kuwatumikia wananchi kwa moyo wote bila ya ubaguzi.
“ Serikali nyingi zilizoundwa na vyama vya
ukombozi duniani zimeangushwa na wakoloni kwa njia za kiutapeli lakini sisi
serikali zetu bado ni imara na zitaendelea kutawala wananchi kwa njia bora na
za kidemokrasia….
Pia ni lazima tuendelee kujitathimini kwa kila
jambo nje na ndani ya chama chetu kwani bado kuna changamoto mbali mbali
zinazotakiwa kufanyiwa kazi ipasavyo”, amesema Dkt. Shein.
Aidha amewasihi wafuasi wa chama hicho na
wananchi kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio
utakaofanyika Machi 20 mwaka huu, ili wapoatikane viongozi wa kuongoza dola kwa
mniaka mitano ijayo.
Dkt Shein amewataka wananchi kuendelea kulinda
Amani na utulivu wa nchi na kuepuka kutumiwa na baadhi ya vyama vya kisiasa
kufanya vurugu sizisokuwa na msingi kwa maslahi ya nchi.
Amefafanua kuwa msingi wa uchaguzi wa marudio upo kikatiba kwani
uchaguzi mkuu uliopita ulifutwa kisheria na mamlaka iliyokuwa inahusika na
usimamizi na uratibu wa uchaguzi huo baada ya kubaini kasoro.
Akizungumzia mgogoro wa kisiasa uliopo Zanzibar, Dkt. Shein amesema
kuwa ulikuwa utatuliwe kwa njia za mazungumzo lakini kiongozi wa CUF ambaye ni
Maalim Seif Sharif Hamad aliyeomba mazungumzo ya maridhiano kabla
hayajamaliza alienda kutoa siri za vikao kwa waandishi wa habari Dar es
saalam na baadae kuandika barua ya kujitoa katika mazungumzo hayo.
Aidha amewataka wananchi kuendelea kulinda Amani na utulivu wa
nchi na kuepuka kutumiwa na baadhi ya vyama vya kisiasa kufanya vurugu
sizisokuwa na msingi kwa maslahi ya nchi.
Akizungumza
katika hafla hiyo Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai amesema kuwa
Zanzibar CCM itaendelea kuwa chama cha wananchi wote kinachoongozwa na
uzalendo.
Amesema kuwa mpaka sasa CCM Zanzibar
imejiandaa kwa kila hatua katika kushiriki kwenye uchaguzi wa marudio
utakaofanyika Machi 20 mwaka huu.
Ally Ndota, Zanzibar
0 comments:
Post a Comment