Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii Tanzania inatarajia kuendesha zoezi la ugawaji wa dawa kwa ajili ya
magonjwa yasiyopewa kipaumbele.
Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika kwa ushirikiano na Ofisi za mikoa mbalimbali na dawa zitakazotolewa kwa Magonjwa ya mabusha,
matende, usubi, trakoma, minyoo, kichocho
na zitatolewa bure kwa wananchi wote kuanzia umri wa miaka mitano hadi kuendelea.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mratibu wa
Kitaifa wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti magonjwa Dkt. Upendo Mwingira alipokuwa akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali
nchini.
Dkt. Mwingira amesema kuwa dawa hizo
zitatolewa kwenye Hospitali, Vituo vya Afya, Zahanati Masoko, Vituo vya Basi,
treni , katika skuli, mashirika ya umma, nyumba za ibada, kambi za jeshi na katika mawizara.
Dkt. Mwingira amesema kampeni hiyo itaanza katika jiji la Dar es
Salaam mwezi huu na katika mikoa mengine ni Katavi, Rukwa, Lindi, Mtwara, Singida,
Dodoma na Pwani.
Ameeleza kuwa katika Mikoa iliyobakia kampeni hiyo itafanyika kwa
awamu kati ya Januari na Februari mwaka huu na dawa zitakazotolewa hazina madhara
yoyote.
MAELEZO-Dar
es salaam
0 comments:
Post a Comment