Wakulima wa zao la
karafuu kisiwani Pemba, wanahofia kushuka kwa mavuno ya zao hilo kutokana na
karafuu kuanza kuanguka kabla ya kipindi cha mavuno.
Hii ni kutokana na karafuu
kuzaliwa katika kipindi cha jua na baadae kunyeshewa na mvua zinazoendelea kabla ya kupevuka.
Wamesema miezi mitatu iliyopita, waliingia na tamaa
kuvuna karafuu nyingi msimu huu hasa kutokana na bei kuwa ya juu lakini kwa
sasa wanaona matumaini yao hayo yamepotea.
Wakizunguma na mwandishi wa habari hizi kwa
nyakati tofauti kisiwani humo wamesema hali hiyo inatishia hasa kwa wale walioamua
kukodi karafuu mwezi mmoja uliopita.
Mmoja kati ya wakulima hao Mohamed Haji wa Wambaa
Mkoani amesema hasara kwa baadhi ya matajiri waliokodi mashamba ya mikarafuu,
imeanza kujitokeza ndani wiki tatu tokea mvua kuanza kunyesha.
Kwa upande wake Hilali Alawi Hija aliekodi shamba la karafuu eneo njia Gando Wete amesema hasumbuliwi na tatizo la wizi lakini amepata mshituko baada ya kugundua kuanguka karafuu kwa wingi.
Kwa upande wake Hilali Alawi Hija aliekodi shamba la karafuu eneo njia Gando Wete amesema hasumbuliwi na tatizo la wizi lakini amepata mshituko baada ya kugundua kuanguka karafuu kwa wingi.
Hata hivyo amesema iwapo zitasita kuanguka ana matumaini
huenda wakarejesha angalau fedha zao walizokodia kwa vile zimeanza kupevuka.
Hata hivyo Mdhamini wa Shirika la Taifa la
Biashara Zanzibar ZSTC, Pemba Abdalla Ali Ussi amesema hali hiyo ni ya kawaida
kujitokeza kama karafuu zitaanza kuzaliwa kwenye msimu wa jua na kisha kupata mvua.
“ Hili lisiwashituwe sana wakulima na matajiri,
maana kuanguka huko kwa karafuu matokeo yake kwa zile zilizobakia huwa na ubora
wa hali juu karibu mara mbili” amesema.
Katika hatua nyengine amesema matarajio kwa mwaka huu kwa Zanzibar
ni kununua tani 3200 za karafuu na tayari tani 580 zimeshanunuliwa lakini kwa mwaka
jana matarajio hayajafikiwa na walinunua tani zisizodizi 250 kati ya tani 895
walizokisia.
Haji Nassor, Pemba
0 comments:
Post a Comment