November 25, 2015


Serikali ya Tanzani kupitia Menejimenti ya Utumishi wa Umma Ofisi ya Rais imesema inaanzisha utaratibu wa kuendesha vikao kazi kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHEMA.
Mfumo huo utawezesha kikao kimoja kuunganisha washiriki kutoka mikoa nane na wajumbe wake kuwasiliana moja kwa moja kwa maswali na ufafanuzi.
Mkuu wa Kitengo cho Mawasiliano Serikalini na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Florence Temba amesema kuanzia sasa  Serikali haitagharamia gharama zozote za kuendesha vikao kazi na watendaji wake badala yake vitaendeshwa Teknolojia hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam amesema kuwa kupitia utaratibu huo washiriki wa vikao hivyo hasa Wakurugenzi, Makatibu Tawala wa Mikoa na Maafisa Utumishi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa watabaki katika maeneo ya kazi na wataunganishwa na mtandao huo.
“ Awali  ilitakiwa lazima watumishi wasafili kuja Dar es Salaam kwa ajili ya mkutano lakini kwa sasa tutatumia Video Conference iliyounganishwa kwenye mikoa yote nchini. tutaokoa gharama za nauli, mafuta, chakula na malazi,” amesema Temba.
Mfumo huo Teknolojia ya Habari na Mawasiliano TEHEMA umeanzishwa na Serikali mwaka 2013/2014 katika mikoa ya Kilimanjaro, Kagera, Morogoro na Iringa kati ya utumishi na mamlaka za Serikali za mitaa na sasa yanapatikana nchi nzima isipokuwa mikoa mipya ya Geita, Simiyu, Katavi na Njombe.

0 comments:

Post a Comment