March 03, 2016

Bodi ya Mapato Zanzibar  ZRB imeshindwa kufikia makadiro ya kukusanya mapato ya zaidi ya sh. billioni 145 na badala yake imekusanya sh. bilioni 125 katika kipindi cha July hadi January mwaka huu.
Tatizo hilo limechangiwa na changamoto mbalimbali ikiwemo wafanya biashara kutotoa risiti kwa wanunuzi wa bidhaa na uingiaji wa bidhaa kwa magendo kupitia bandari bububu.
Meneja wa huduma kwa wateja wa bodi hiyo Ahmed Haji Saadat  akizungumza katika semina ya waandishi wa habari juu ya umuhimu wa kulipa kodi amesema bodi hiyo kitendo hicho kinaikosesha mapato serikali.          
Meneja huyo amesema katika kulithibiti tatizo hilo ZRB kwa kushirikiana na jeshi la polisi inafanya msako katika bandari hizo pamoja na vituo vinavyouzwa mafuta ili kuwabaini wanaokwenda kinyume na utaratibu uliowekwa. 

0 comments:

Post a Comment