Mamalaka
ya Mawasiliano Tanzania TCRA imezitoza faini ya Sh. Milioni 90 Kampuni tano
za Mawasiliano ya Simu za Mkononi kutokana
na kushindwa kutimiza masharti ya kanuni za ubora wa huduma.
Kampuni
hizo ni Aitel imetozwa sh. milioni 22.5, Smart sh. milioni 12.5, Tigo
sh.milioni 25,Vodacom sh. milioni 27.5 pamoja na Zantel sh.milioni 25.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dk.Ally Simba amesema kampuni hizo
zimepigwa faini tofauti kutokana na makosa mbalimbali ya utoaji huduma ya mawasiliano
kwa wananchi.
Dk.Simba amesema kampuni ziliitwa na mamlaka na zilikiri kufanya hivyo na kukubali na kosa na kuafiki maamuzi ya kuwapiga faini kwa mujibu wa sharia za nchi.
Dk.Simba amesema kampuni ziliitwa na mamlaka na zilikiri kufanya hivyo na kukubali na kosa na kuafiki maamuzi ya kuwapiga faini kwa mujibu wa sharia za nchi.
Ametaja
baadhi ya makosa hayo ni simu iliyopiga kudai kuwa inatumika wakati sivyo,
wakati mwingine simu unapiga mwito wake unadai simu hiyo haipatikani wakati
simu hiyo iko hewani.
Amesema
kuwa kutokana kampuni hizo kushindwa kutimiza masharti TCRA itaendelea na
utekelezaji wa sheria na maamuzi mengine kwao kwa mujibu wa sheria zilizowekwa.
Dk.Simba
amesema kuwa kampuni za simu za mikononi zimejikita katika kujitangaza kwa njia
mbalimbali katika kuweza kupata wateja wapya lakini hazifanyi uwekezaji wa
huduma bora kwa wananchi wanaotangazia.
Katika
hatua nyengine TCRA imeipiga faini kampuni ya Azam Marine Sh.Milioni Tano
kutokana na kufanya usafirishaji wa vifurushi kutoka Dar es Salaam na Zanzibar
bila kuwa na leseni ya utoaji wa huduma hiyo.
Amesema
kuwa ni kosa kwa Azam Marine kufanya huduma ya posta bila kuwa leseni huku
wakikri kufanya biashara ya kusafirisha vifurushi.
Kampuni
nyengine ni ya Lifalo imetozwa faini sh.milioni 10 kutokana na kufanya masafa
ya ujumbe mfupi bila kuwa na kibali cha TCRA na lifalo ilikiri kufanya hivyo.
Watendaji wa TCRA na waandishi habari
wakisikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TCRA,
Dk. Ally Simba (hayupo pichani) leo
jijini Dar es Salaam.
|
0 comments:
Post a Comment