March 01, 2016

Zoezi la Upigaji dawa Majumbani kwa ajili ya kuuwa mbu waenezao Malaria  limenza  rasmi kisiwani Pemba ambapo Jumla ya Nyumba 31,369 zitapulizwa Dawa  katika Wilaya ya Micheweni na Wilaya Ya Chake chake.
Taarifa zilizotolewa na Mratibu wa Kitengo cha Upigaji dawa  Kisiwani Pemba Khamis Salim amesema  zoezi  hilo  litafanyika  katika Shehia 4 za Wilaya ya Michweni na Shehia Moja Wilaya ya Chake kuanzia tarehe 1/3/2016 hadi tarehe 14/3/2016 na linaendeshwa na Shirika la ABT la Marekani kwa kushirikiana na Kitengo cha kupambana na Malaria Zanzibar (ZAMAP)  linanza Rasmi .
Amezitaja shehia zinazohusika ni Makangale ,Mgelema, Tumbe Mashariki, Chimba na Shumba vyamboni.
 Mratibu Salim amesema kuwa  kigezo  kikubwa  kilichotumika  kuzipuliza dawa  shehia hizo ni kesi nyingi zilizopatikana  katika Maeneo hayo yaliyokuwa sugu  katika kupambana na Malaria , licha ya Juhudi kubwa  zinazochukuliwa  kukabiliana  na hali  hiyo.
Amewaomba  wananchi kushirikiana  na wapiga dawa majumbani kwa kuruhusu nyumba zao kupigwa  dawa  vyumba vyote na waache tabia  ya ujanja  wakutaka wapigiwe dawa baadhi ya vyumba pekee.
Mratibu Salim amefahamisha kuwa zoezi hilo  haliwezi  kufanikiwa  iwapo Wananchi tasisi za Serikali na asasi  za kiraia  hawatotoa ushirikaiano wao wa dhati  katika  kuitokomeza  malaria ambayo imekua ikisababisha  vifo vingi   hasa watoto chini ya umri wa miaka mitano

0 comments:

Post a Comment