Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein amesema juhudi kubwa
zilizochukuliwa na serikali katika kuimarisha miundombinu ya sekta ya
afya zimefanikisha utoaji wa huduma za matibabu
kwa wananchi mijini na vijijini.
Amesema hatua hiyo inatoa
fursa nzuri kwa wananchi kupata huduma za uhakika za afya bila ya
usumbufu ikilinganishwa na zilivyokuwa zikitolewa miaka michache iliyopita.
Dr. Shein amesema hayo katika
hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano wa tathmini
ya mapitio ya pamoja ya sekta ya afya iliyosomwa na makamu wa pili wa rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi nje kidogo ya mjini Zanzibar.
Amefahamisha kuwa hatua hizo
ina lengo la kuona huduma za afya zinapatikana kwa wananchi si zaidi ya
kilomita tano karibu na maeneo wanayoishi hasa vijijini.
Hata hivyo Dr. Shein ameeleza
kuwa ujenzi wa majengo mapya ya afya na uwepo wa vifaa bora vya matibabu
hautatimia iwapo mipango ya muda mfupi na mrefu haitawekwa katika kuwapatia
taaluma ya kisasa watendaji wa sekta hiyo muhimu.
Akigusia upatikanaji wa
dawa mbali mbali Dr. Shein amesema katika serikali ya Zanzibar imeongeza bajeti kutoka Shilingi bilioni 1.0
hadi Shilingi bilioni 4.3 mwaka 2015/2016 ili kukabiliana na upungufu wa huduma
hiyo.
Dr. Shein ameishauri Wizara ya Afya kuendelea
kusimamia vyema mipango iliyoiweka
ikiwemo ile inayofadhiliwa na washirika
wa maendeleo ambayo itawawezesha watendaji wa sekta hiyo kutoka huduma kitaalamu
zaidi.
Amewataka washiriki wa
mkutano huo wa mapitio ya pamoja ya sekta ya afya wakiwemo
madaktari waliobobea, wataalamu wa masuala ya mazingira wa ndani na nje ya nchi
kutumia nafasi yao kitaalamu katika kutathmini sekta hiyo na kutoa ushauri na muongozo yao katika kufikia viwango
vinavyokubalika kitaifa na kimataifa..
Mapema Mwakilishi wa
Taasisi na Mashirika Hisani ya Kimataifa yanayotoa huduma Nchini Tanzania Dr.
Christin Harmel aMEsema ni muhimu hudujma
za afya ya msingi lazima ziendelee kuimarishwa ili kuwa na jamii yanye afya na
uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji mali
utakaosaidia mapato ya taifa.
Amesisitiza watendaji wa
afya kuhakikisha kila motto anayezaliwa
mikononi mwao ni lazima alindwe, ahifadhiwe na kutunzwa katika mazingira bora
yatakayomuwezesha kukua kwa amani na upendo.
Akimkaribisha mgeni rasmi
kuufungua Mkutano huo Naibu Waziri wa Afya
Zanzibar Mh. Mahmoud Thabit Kombo aMEyashukuru Mashirika na Taasisi za Kimataifa na zile za Kitaifa Kwa mchango wo mkubwa ulioiwezesha Wizara ya Afya kufanya kazi zake kwa ufanisi mkubwa.
Zanzibar Mh. Mahmoud Thabit Kombo aMEyashukuru Mashirika na Taasisi za Kimataifa na zile za Kitaifa Kwa mchango wo mkubwa ulioiwezesha Wizara ya Afya kufanya kazi zake kwa ufanisi mkubwa.
Mkutano huo unaozungumzia
tathmini ya mapitio ya pamoja ya Sekta ya Afya Zanzibar umeoshirikisha
Wataalamu na Washirika wa Maendeleo kutoka Taasisi za Kimataifa na Kitaifa umefadhiliwa
na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) kwa kushirikiana na
Wizara ya Afya.
Mwakilishi wa Taasisi na Mashirika Hisani ya Kimataifa yanayotoa
huduma za afya Nchini
Tanzania Dr. Christin Harmel akitoa salamu
kwenye Mkutano wa
Tathmini ya mapitio ya Sekta ya Afya.
|
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dr. Saleh Mohammed Jidawi akitoa
maelezo ya ufafanuzi kwenye Mkutano wa Tathmini ya mapitio
ya Sekta ya Afya hapo Zanzibar Beach Resort Mbweni.
|
Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa mashirika na taasisi za Kimataifa na zile za kitaifa zinazotoa huduma ya Afya Zanzibar. |
0 comments:
Post a Comment