Bodi ya Chakula Dawa na Vipodozi inajukumu
kubwa la kuhakikisha kuwa Dawa zinazoingia nchini ni salama na zinafaa kwa
matumizi ya mwanadamu.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Bohari kuu ya
dawa Zahran Ali Hamad wakati akifungua mkutano wa siku tano wa udhibiti wa dawa
kwa wafamasia wa hapa nchini.
Amesema ni vyema wafamasia hao kutumia
taaluma walinayo ili kuhakikisha wanadhibiti uingiaji wa dawa zisizo na viwango
kwa lengo la kumkinga watumiaji na maradhi mbali mabali yanayotokana na dawa.
Amewataka wafamasia hao kuongeza jitihada
katika suala zima la udhibiti wa dawa wakati zinapoingia nchini kwa kuwezesha
kuepuka matatizo ya afya za wanaadamu.
Alisema hivi sasa Tanzania ni miongoni mwa
Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni vyema kuongeza ushindani wa utoaji wa
huduma bora kwa jamii na kuhakikisha kuwa Zanzibar haiingizi dawa bandia.
Mrajis wa Bodi ya Chakula Dawa na vipodozi Dk
Burhan Othman Simai amesema kuwa katika mpango mkakati wao ni kuwapatia mafunzo
wafanyakazi wake ili kuweza kukabilina na mabadiliko yanayotokea ulimwenguni
Amefahamisha kuwa katika kukabilina na hali
iliyopo hivi sasa ni vyema Serikali kuongeza wafanyakazi wa kada ya ufamasia
ili kuweza kufanyakazi kwa ufanisi katika sehemu tofauti.
Alisema wataendeleza mafunzo kwa wafanyakazi
wake ili kwenda sambamba na haja iliyopo na katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mapema mkufunzi wa usajili wa Dawa kutoka
Mamlaka ya Chakula Tanzania David Robert Matle amesema ni vyema dawa kuifanyia
usajili kwa kutimiza vigezo vya ubora, usalama wa dawa hizo.
Amesema lengo la usajili wa dawa ni kuwalinda
wanaadamu wasipate madhara yanayotokana na dawa.
Picha ya pamoja ya washiriki wa Mafunzo ya siku tano ya udhibiti
wa
Dawa, yaliyoandaliwa na Bodi ya
Chakula Dawa na Vipodozi Zanzibar.
Picha -Maelezo Zanzibar.
|
0 comments:
Post a Comment