March 11, 2016

Karatasi za kupigia kura kwa ajili ya uchaguzi wa marejeo wa Machi 20, 2016 zimewasili Zanzibar zikitokea nchini Afrika ya kusini.
Kura hizo utengezaji wake umegharimu Sh. bilioni 4.5 kwa ajili ya idadi ya wapiga kura ambayo ni 53800.

Karatasi hizo zimewasili majira ya saa nane mchana katika uwanja wa ndege wa Zanzibar baada ya kuteremshwa zimepelekwa ghalani kuhifadhiwa zikisubiri tarehe ya kusambazwa.
Viongozi viongozi mbali mbali wameshuhudia akiwemo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salim Jecha na baadhi ya Makamishna wa Tume hiyo, pamoja na viongozi wa vyama vya Siasa kikiwemo cha TADEA, CCM na baadhi ya waangalizi wa ndani wa vyama .
Mkurugenzi wa ZEC Salum Kassim Ali, amesema pia wamepokea vifaa vya nukta nundu elfu 2000 kwa ajili ya watu wasioona, na wanatarajia kuanzia Machi 17 zitasafirishwa kisiwani Pemba na siku inayofuata ya  Machi 18 zitaanza kugawia katika Wilaya za Unguja.





0 comments:

Post a Comment