Karatasi za kupigia kura kwa ajili ya uchaguzi
wa marejeo wa Machi 20, 2016 zimewasili Zanzibar zikitokea nchini Afrika ya kusini.
Kura hizo
utengezaji wake umegharimu Sh. bilioni 4.5 kwa ajili ya idadi ya wapiga kura
ambayo ni 53800.
Karatasi hizo zimewasili majira ya saa nane mchana
katika uwanja wa ndege wa Zanzibar baada ya kuteremshwa zimepelekwa ghalani
kuhifadhiwa zikisubiri tarehe ya kusambazwa.
Viongozi viongozi mbali mbali wameshuhudia
akiwemo Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salim Jecha na baadhi ya
Makamishna wa Tume hiyo, pamoja na viongozi wa vyama vya Siasa kikiwemo cha
TADEA, CCM na baadhi ya waangalizi wa ndani wa vyama .
Mkurugenzi wa ZEC Salum Kassim Ali, amesema pia
wamepokea vifaa vya nukta nundu elfu 2000 kwa ajili ya watu wasioona, na
wanatarajia kuanzia Machi 17 zitasafirishwa kisiwani Pemba na siku inayofuata
ya Machi 18 zitaanza kugawia katika
Wilaya za Unguja.
0 comments:
Post a Comment