Tume
ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC imesema maandalizi ya uchaguzi wa marudio wa tarehe
20 machi 2016 yamefikia hatua nzuri na kazi ya uchapishaji wa daftari la wapiga kura
itakuwa imekamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi huu.
Taarifa
iliyotolewa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Jecha Salim Jecha imesema kuwa madaftari
ya wapiga kura ya nje ya vituo yatabandikwa wiki moja kabla ya uchaguzi
ili kuwapa nafasi wapiga kura kuelewa vituo walivyopangiwa.
Ameyataja
matayarisho mengine yaliyokuwa katika hatua nzuri kuwa ni pamoja uteuzi wa
wasimamizi wa Majimbo, upangaji wa vifaa na vituo, pamoja na mafunzo kwa
watendaji.
Jecha
ameongeza pia matayarisho ya awali ya
uchapishaji wa karatasi za kura yamekamilika baada ya tume kumpitisha
mchapishaji wa karatasi hizo na zinatarajiwa kuwasili nchini mwanzoni mwa mwezi
wa Machi.
Akizungumzia
mawasiliano kwa vyama vya siasa na wagombea Jecha amesema kuwa tume itaendelea
kuwahesabu wagombea wote wa uchaguzi uliopita ni halali kutokana na kutofuata
utaratibu wa kisheria za kujitoa kwa
wagombea.
Ameeleza
kuwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi nambari 11 ya mwaka 1984 sura ya tatu
kifungu cha 31 hadi 37a kinatoa sharti la kuwepo wadhamini wa wagombea na hakuna
chama kilichoiandikia tume kuwa kimefuta udhamini wa wagombea wake kushiriki
katika uchaguzi huo.
HII HAPA TAARIFA KAMILI YA ZEC
0 comments:
Post a Comment