Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar imesema itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na sekta binafsi
za kuwasaidia wananchi miradi
mbali mbali ya kimaendeleo inayofanywa kwa nia ya kupunguza umaskini katika
jamii.
Kauli hiyo imetolewa na
Naibu Katibu mkuu Wizara ya Afya Zanzibar , Halma Maulid Salim wakati
akikabidhiwa vifaa vya Hospitali na Shirika la misaada ya kijamii la Helping Hand
kutoka Marekani, huko katika skuli ya Muzdalifah Islamic Charitable Organization(MICO)
Zanzibar iliopo Mitondooni Kisauni.
Ameeleza kuwa taasisi
binafsi zimeweza kuisaidia serikali katika kufanya miradi na kuomba misaada
mbali mbali ya maendeleo ili iwanufaishe wananchi wengi hasa wanaoishi vijiji.
Bi, Halima amesema vifaa
hivyo vitasaidia utoaji wa huduma bora za kiafya nchini katika Vituo vya afya vitakavyonufaika
na msaada huo ili kuhakikisha kila
mwananchi anapata huduza za uhakika.
Vifaa vilivyotolewa ni
pamoja na vigari vya watu wenye ulemavu 6, vitanda vya hospitalini 6, kitanda
cha wagonjwa mahututi 1, vitanda
vya dharura 2, mipira ya haja ndogo 2000, visaidizi vya kutembelea kwa watu
waliopata ajali 40, miguu bandia ya watu wenye ulemavu pamoja na viatu vyote
vikiwa na thamani ya Dola za kimarekani 345,320.
Akikabidhi vifaa hivyo
Mwakilishi kutoka Helping Hand kutoka Marekani, Mohammed Habibu amesema msaada
huo ni miongoni mwa fursa zinazotolewa na shirika hilo kwa nchi mbali mbali
duniani zinazokabiliwa na upungufu wa vifaa vya kisasa katika utoaji wa huduma
za afya kwa wananchi.
Ameeleza kuwa kutokana na
sifa ya Zanzibar na watu wake shirika hilo litaendelea kuweka mipango endelevu
ya kuhakikisha watapata misaada katika sekta mbali mbali kwa kuzingatia mahitaji
ya wananchi.
Kwa upande wake Katibu
Mkuu wa Jumuiya ya Muzdalifah Islamic Charitable Organization(MICO), Farouk
Hamad amesema vifaa hivyo ni miongoni mwa matunda ya miradi ya kusaidia jamii
ya Zanzibar inayoombwa na
jumuiya hiyo kwa wahisani mbalimbali.
Ameeleza kuwa licha ya
jumuiya hiyo kubuni miradi mbali mbali ya kuisaidia jamii katika nyanja za
kiuchumi na kijamii bado wanawabiliwa na changamoto ya ukosefu wa dawa katika
kituo cha afya kinachomilikiwa na jumuiya hiyo, pamoja na upungufu wa
wafanyakazi kutokana na ufinyu wa vyanzo vya mapato.
0 comments:
Post a Comment