February 27, 2016

Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar kwa kushirikiana na kitengo cha polisi wa kimataifa Interpol na kampuni ya kimataifa ya ushauri wa kulinda Alama za biashara Brand Protection Agency linaendelea na uchunguzi kuhusu Kontena lenye urefu wa futi 40 lenye DVD 1,0310 zisizokidhi viwango ambazo zinadaiwa kubeba jina la SINGSUNG.
Kontena hilo ni lenye namba PCIU888100 (1) Seal Namba T. 093094 PIC lililosafirishwa na meli ya MV. Kota Harmut kutoka nchini China lilikamatwa katika bandari ya Zanzibar.
 Akizungumza na wanahabari visiwani Zanzibar wakati akitowa taarifa ya matukio mbali mbali  Naibu mkurugenzi wa upepelelezi wa makosa ya jinai Zanzibar Salum Msangi amesema kuwa upelelezi utakapokamilika watafikisha kesi hiyo mahakamani kuendelea na utaratibu ikiwa lengo ni kutokomeza bidhaa zisizo na viwango na kuifanya nchi kama jaa la bidhaa mbovu.
Aidha kamanda Msangi amesema kuwa  pamoja na hali hilo wanaendelea kumshikilia Mtu mmoja anaedaiwa kutowa CLIP yenye lugha za matusi dhidi ya Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dr Ali Mohammed Shein katika mitandao ya kijamii huku wakiendelea kuwafuatilia wengine ambao wameeleza wanawafahamu.
Amesisitiza upana wa demokrasia isiwe sababu ya kufanya uhalifu na jeshi lipo macho zaidi kwa watu hao
Aidha kamanda amezungumzia njia mpya ambayo inatumika kusafirishia madawa ya kulevya hasa pale walipokamata kasha 3 zenye ukubwa tofauti zenye uzito wa kilo 18 zilizotoka Adisababa Ethiopia zenye majani ambayo kiutafiti yakiwekwa katika maji hugeuka na kuwa mirungi.
Pamoja na mambo mengine amevitaka vyombo vya habari kuendelea kufanya utafiti wa habari zao kwa kila kilichojitokeza  baadhi ya vyombo hutowa taarifa zisizo sahihi.

0 comments:

Post a Comment