February 05, 2016

Jaji Mkuu wa Zanzibar Jaji Omar Othman Makungu amesema mbali na makosa ya mitandao yanafanywa na watu kadhaa Zanzibar bado mahakama haina  uwezo wa kuyashughulikia kutokana sheria ya makosa hayo Tanzania haijaanza kutumika rasmi.
Amesema sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili iweze kufanya kazi Zanzibar lazima iridhiwe na baraza la Wawakilishi.
“ Hili suala bado hadi sasa halijafanyika ndo tunasubiri wapitishe ili tuweze kuanza kuzishughulikia kesi za aina hiyo na kuzitolea hukumu”. amesema Jaji Makungu.
Alikuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya siku ya sheria yanayofikia kilele chake Februari 10, 2016 yakiwa na  kauli mbiu Matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii yanaweza kuwa chanzo cha uvunjaji wa sheria na amani ya nchi..
Jaji makungu   amesema sheria hiyo imeanza kutumika Septemba 1, 2015 wakati Baraza la Wawakilishi lilikuwa limeshavunjwa na hivyo kulikuwa na ugumu kuridhiwa.

Akizungumzia kuhusu maadhimisho hayo kwa Zanzibar yataambatana na   uwekwaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa mahakama mpya ya watoto huko Mahonda pamoja na kuifanyia matengenezo mahakama kama hiyo huko Pemba.

Rais wa Wanasheria Zanzibar Omar Saidi akitoa ufafanuzi kuhusu
 jumuiya hiyo inavyotoa huduma za kisheria kwa wananchi
kwenye mkutano ulioitishwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar
uliozungumzia wiki ya sheria Zanzibar

0 comments:

Post a Comment