February 10, 2016

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein amesema kila mtu anajukumu la kuelimisha Jamii kuhusu utamiaji wa matumizi ya mitandao ya Kijamii kueleza faida na hasara zake.
Amesema ipo baadhi ya mitandao hiyo inatumiwa kurusha habari za uchochezi na uongo dhidi ya serikali huku wakijua taarifa wanazozituma zinapingana na sheria na maadili ya nchi.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya sheria katika viwanja vya Victoria Garden Dkt amefahamisha kuwa ingawa kila mtu sheria zimeonesha kua kila mtu ana haki ya kupata habari na kutoa habari bila ya kubughudhiwa lakini taarifa hiyo isivunje sheria zilizo wekwa.
“Mitandao  ni nyenzo muhimu katika maisha ya Binaadamu iwapo itatumika vizuri haitakuwa na hasara hivyo kuna haja kwa kila mmoja kuelimisha jamii yake umuhimu wake na hasara zake”amesema Dkt Sheni.
Ameeleza kuwa Tanzania imetunga sheria ya mitandao ya mwaka 2015 yenye lengo la kuimarisha matumizi bora kwa kuainisha makosa yanayohusiana na matumizi ya teknolojia ya habari.
Amesema sheria hiyo itaanza kutumika Zanzibar baada ya kuridhiwa na Baraza la Wawakilishi hivyo ametoa wito kwa taasisi zinazohusika na utoaji taaluma ya sheria kuongeza kasi ya kuwa elimisha wananchi juu ya sheria hiyo mpya.
Amewahimiza majaji, mahakimu, wanasheria na jeshi la polisi kuisoma sheria hiyo na kuielewa ili waweze kutoa mchango wao katika kuitekeleza  kwa mujibu wa majukumu na nafasi zao.
Kuhusu uimarishaji wa huduma za mahakama  Dkt  Shein ameahidi kuwa ujenzi wa mahakama kuu mpya unaotarajiwa kufanyika huko Tunguuu Mkoa wa kusini Unguja utaaanza katika mwaka ujao wa fedha.
Amefahamisha kuwa bajeti ijayo ujenzi wa mahakama hiyo utaanza bila pingamizi yoyote sambana na ujenzi wa mahakama ya watoto tayari wametengewa milioni 30 za kukamilisha jengo hilo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akifuatana na Jaji Mkuu wa
Zanzibar Omar Othman Makungu (kulia) na Jiji Mkuu Tanzania 
Mohammmed Chande Othman alipowasili viwanja vya Victoria
Garden katika sherehe za kilele cha siku ya sheria Zanzibar.

Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu akitoa hutuba 
yake wakati wa sherehe za kilele cha siku ya sheria Zanzibar 
kabla ya kumkaribisha Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza 
la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein kuzungumza na wananchi
 katika sherehe za siku hii ya sheria. (picha Ikulu)


0 comments:

Post a Comment