Wizara ya Kilimo na Maliasili Zanzibar imesema kuna hatari ya
kuwepo mavuno kidogo ya mpunga katika msimu huu kufuatia uchelewaji wa matayarisho
ya mashamba kwa ajili ya kilimo hicho.
Naibu katibu mkuu wa kilimo Juma Ali Juma amesema maeneo mengi ya mashamba hayo hayajafikiwa na kutokana
na wakulima kushindwa kuchangia huduma za matrekta.
Amewaambia waandishi wa habari kuwa katika msimu huu wa kilimo wanatarajia kulima
ekari elfu 33 lakini hadi sasa ni ekari elfu tisa pekee ndio zimehudumiwa
katika vijiji vya mtende na muyuni mkoa kusini Unguja.
Amesema ingawa wizara hiyo inakususida kutoa pembejeo kwa
wakulima ikiwemo mbolea, dawa za kuulia magugu na mbegu lakini bado mwamko wa wakulima
ni mdog.
Katika hatua Wizara ya Kilimo na Maliasili imeandaa mkakati
wa kurejesha kilimo cha asili kisichotumia dawa na mbolea zenye kemikali ikiwa
ni juhudi za kuimarisha kilimo cha asilia Zanzibar.
0 comments:
Post a Comment