February 06, 2016

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi  Taifa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema chama hicho kimelazika kukubaliana na maamuzi ya Tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC kwa kuwa ndiyo yenye mamlaka ya kufanya hivyo.
Amesema CCM ilitamani kusingekuwepo na marudio ya Uchaguzi visiwani Zanzibar kwa kuwa maandalizi ya kuuandaa ni kazi nzito na inatumia gharama kubwa hadi kufanyika.
Tulikuwa tumejiandaa kushangilia, lakini Tume wakasema kuwa uchaguzi unafutwa kwa kuwa kulikuwa na dosari kubwa, tukasikitika sana lakini kwa kuwa tume wameamua, tukashauriana na wenzetu wa Zanzibar, tukaona ni bora kukubali kurudia uchaguzi huo, lakini hatukupenda”
Amewaomba wanachama wa chama hicho Zanzibar kujiandaa kikamilifu kushiriki uchaguzi huo wa marudio  hapo 20 Machi 2016 kama ilivyoelekezwa na ZEC kwani  ndio njia pekee ya kuiwezesha kupatikana demokrasia kufuatia ule wa awali kuwa na kasoro kadhaa.
Akizungumza katika maadhimsho ya kutimia miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi  Mkoani Singida  Dkt Kikwete ambae pia ni rais msataafu wa Tanzania  amesmema chama hicho ndicho chenye uwezo wa kusimamia  mageuzi na mabadiliko  ya kweli na kitaendelea kuimarika na kukubaliwa na wananchi huku kikijihakikishia ushindi mwaka   2020.
Nae Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  amewaagiza viongozi  wa ngazi zote  wakiwemo  wa mikoa  na wilaya kutumia vyeo vyao katik kuhakikisha wanaondoa kero zinazowakabili wananchi kulingana na matakwa ya ilani ya CCM inayochoongoza nchi kwa sasa.

Akitoa salam zake katika sherehe hizo, amesema tayari serikali itaendelea kuyafanya kazi kikamilifu ikiwemo  kuwabaini wazembe na mafisadi "kutumbua majipu" kwa maslahi  ya watanzania bila kujali vyama vyao.
“Nawaeleza watendaji wote serikalini kuwa atakayeshindwa kufanya kazi, nitamueleza kwa upole sana maana mimi ni mtu mpole, nitamuambia akae pembeni apishe wengine”
Rais Magufuli pia ametumia nafasi hiyo kukishukuru Chama cha Mapinduzi kufanikisha yeye kuwa Rais kwa kuwa bila chama hicho yeye asingelipata nafasi hiyo.
“Nataka watanzania wote wajue kuwa bila CCM mimi nisingekuwa Rais wao, kwa hiyo huwezi kunitenganisha mimi na CCM, ndiyo maana leo nimekuja nimevaa kijani yangu hapa na sioni kama kuna chama kingine chochote kitakachokuja kutawala Tanzania zaidi hiki”

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais Mstaafu wa Jamhuri
 ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akipokelewa na 
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana alipowasili kwenye
 maadhimisho ya miaka 39 ya CCM yanayofanyika kwenye 
uwanja wa Namfua mjini Singida


Rais Dk. John Pombe Magufuli akiwapungia mikono wana CCM
na wananchi wakati alipowasili kwenye uwanja huo.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Move waliohudhuria katika maadhimisho
 hayo kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.

0 comments:

Post a Comment