Waziri wa Afya ,Maendeleo
ya Jamii, Jinsia,Watoto na Wazee Ummy
Mwalimu amewasimamisha wakurugenzi toka Bohari ya Dawa ya Taifa(MSD) kwa
ubadhilifu wa fedha takribani Shillingi Billion 1.5.
Wakurugenzi
hao wa Bohari ya dawa MSD ni pamoja na Mkurugenzi wa kanda huduma
kwa wateja Cosmas Mwaifwani, Mkurugenzi wa fedha Joseph Tesha, Mkurugenzi wa
ugavi Misanga Muja na Mkurugenzi wa manunuzi Henry Mchunga.
Akizungumza na Waandishi
wa Habari katika Kitengo cha Afya ya Mama na Mtoto baada ya
kupokea vifaa toka Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa (MSD) amesema amepata
taarifa ya uchunguzi ofisini kwake ya ubadhilifu wa kiasi hicho cha fedha na
kuamua kuwasimamisha wakurugenzi wanne kupisha uchunguzi.
Amewataja viongozi hao ni
Joseph Tesha Mkurugenzi wa Fedha na Mipango, Misanga Muja Mkurugenzi wa Ugavi,
Heri Mchunga Mkurugenzi wa Manunuzi na Cosmas Mwaifani Mkurugenzi Kanda na
Huduma kwa Wateja na amewataka Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Bodi ya Bohari ya
Dawa ya Taifa kuwaandikia barua mara moja ya kuwasimamisha kazi.
“ Nimeletewa taarifa
ofisini kwangu na nimeamua kuchukua fursa hii kuwaambia na hili pia kwamba
nimewasimamisha wakurugenzi wanne toka Bohari ya Kuu Dawa ya Taifa kwa
ubadhilifu wa fedha na nisingeweza kusubiri nitumbuliwe mimi jipu na Mhe. Rais
kwa hiyo nimeamua kuwachukulia hatua kwa kuwasimamisha kazi ili
kupisha uchunguzi”
“ Hizi ni zama za kufanya
kazi na kuwajibika sasa inabidi tuwajibike kwa kufanya kazi na hatutowavumilia
watendaji watakaoenda kinyume na utaratibu katika ofisi yoyote ile katika sekta
ya afya na tutawachukulia hatua kwani tunataka uwajibikaji ili kuiendeleza
sekta ya afya ambayo ni muhimu sana kwa kila mwanadamu” amesema
Ummy.
Katika kuboresha sekta ya
afya nchini Wizara wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee
imejipanga kufanya kazi kwa taratibu na misingi iliyopo ili
kuhakikisha inapeleka mbele gurudumu la maendeleo ya hasa katika sekta ya afya
kwa ujumla.
0 comments:
Post a Comment