February 12, 2016

Chama cha Wakulima (A.F.P) kimesema kitashiriki uchaguzi wa marejeo wa Zanzibar huku kikilaani watu wanaotaka kufanya fujo siku ya kufanyika uchaguzi huo  tarehe 20 machi mwaka huu   
Hayo ameyasema na Mgombea wa Urais wa chama hicho Said Suod huko Vuga Mjini Zanzibar katika ukumbi wa Cultuer wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu  tamko la kushiriki kwa  uchaguzi kwa ngazi zote.
Amesema chama chake kitashiriki uchaguzi bila yakufanya fujo na kuheshimu sheria zote zilizowekwa katika uchaguzi ili kuweza kufanikisha kufanyika uchaguzi huo kwa  amani.
Amesema kuwa uchaguzi uliofanyika tarehe 25/10/2015. Ulifutwa kihalali kutokana na udanganyifu uliofanyika . na kupelekea kuhairishwa kwa uchaguzi  huo na kutajwa tarehe ya kurejewa uchaguzi.
Hata hivyo amefahamisha zaidi watu waliosababisha udanganyifu na kupelekea kufutwa kaw uchaguzi ni vyema wakachukuliwa hatua ili wasijerejea kutokea kwa ubadhilifu mwengine.
Aidha amewaomba viongozi wakuu wa Serikali kuzidisha ulinzi siku ya uchaguzi li kuweka utulivu katika nchi na kuepusha kutokea kwa vurugu zitakazo sababish uvunjifu wa amani
Sambamba na hayo amewaomba wazanzibar wote kushiriki uchaguzi na kuwachaguwa wagombea kwa ngazi zote za udiwani, urais na uwakilishi bila kuleta fujo ya aina yoyote.





:Maelezo Zanzibar.

0 comments:

Post a Comment