Chama Cha National Reconstruction
Alliance (NRA) kutoka Zanzibar kimethibitisha kushiriki uchaguzi wa marudio wa
Zanzibar unaotarajiwa kufanyika Machi 20, mwaka huu baada ya kikao
kilichofanyika Februari 15.
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu
Tanzania Bara Hassan Almasi Kisabya alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari leo jijini Dar es salaam ambapo amesema kuwa Chama hicho kitashiriki
uchaguzi wa marudio na kusisitiza kuwa tamko lililotolewa na mgombea wao la
kutoshiriki uchaguzi wa marudio lipuuzwe kwani ni tamko lake binafsi na sio
msimamo wa chama.
“Tamko lililotolewa tarehe
14/02/2016 Si Tamko la chama cha NRA bali ni tamko binafsi na wale waliomuagiza
kwani yeye hana mamlaka ya kukisemea chama wala wagombea wengine wa chama
pasipo Baraka na vikao halali vya chama” alisema Kisabya.
Amesisitiza kuwa maamuzi ya chama ni
sharti yatoke katika chama na sio kwa mgombea na ikiwa yeye amejitoa anatakiwa
afuate taratibu za kisheria katika kujitoa kama alivyofuata sheria katika
kugombea nafasi hiyo.
Aidha, Chama kinatoa taarifa kwa wagombea wote Zanzibar kujiandaa na wapiga kura kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20, mwaka huu ili kutimiza haki yao kikatiba na kuchagua viongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Aidha, Chama kinatoa taarifa kwa wagombea wote Zanzibar kujiandaa na wapiga kura kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20, mwaka huu ili kutimiza haki yao kikatiba na kuchagua viongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Maelezo
DSM
0 comments:
Post a Comment