Kazi za usafi wa mazingira kwenye maeneo
tofauti Nchini zimefanyika ikiwa ni kuanza rasmi maadhimisho ya sherehe za
kutimia miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar
Wananchi kadha wameonekana kuitikia vyema sughuli
hiyo pamoja na vikosi vya ulinzi Nchini walishiriki.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif
Ali Iddi alijumuika na Wananchi hao kwa kazi za usafishaji wa Mtaro wa maji
machafu unaokusanya maji kutokea mitaa ya Muembe Njugu, Kwahani, Kariakoo,
Kilimani na Kumalizikia Pwani ya Kilimani.
Wapiganaji wa Vikosi vya Mafunzo, Jeshi la
Kujenga Uchumi, Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo, Zimamoto na Uokozi, Valantia,
vikundi vya usafi wa mazingira vilivyomo ndani ya Wilaya ya Mjini,
watendaji wa Baraza la Manispaa na Wananchi walionekana kuhamasika katika
harakati hizo.
Afisa Uhusiano wa Baraza la Manispaa
Zanzibar Moh’d Nassor Ali alieleza Baraza hilo limeanzisha mradi maalum
wa kuimarisha Miundombinu katika uchimbaji wa mitaro { ZUSP } ndani ya Manispaa
ya Mji wa Zanzibar wa lengo la kuujengea mazingira mazuri katika miendendo ya
maji machafu.
Amesema hatua hiyo kwa hivi sasa
inaendelea katika eneo la Mtaa wa Mpendae { Maarufu kwa Binti Hamrani } kwa
ujenzi wa Mtaro mkubwa kazi inayokwenda sambamba na ujenzi wa mtaro kama huo
katika Uwanja wa Michezo wa Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar.
Akizungumza na washiriki wa zoezi hilo la
usafi wa mazingira Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewapongeza
Wananchi pamoja na Vikosi vya ulinzi kwa ushiriki wao wa usafi wa mazingira.
Balozi Seif amesema kwa vile Zanzibar
imefanikiwa vyema katika kuangamiza Maradhi ya Malaria kwa asilimia 99% hakuna
sababu nguvu na hamasa kama hiyo Wananchi kuchukuwa juhudi ya
kuielekeza katika usafi wa mazingira kwenye maeneo wanayoishi.
Katika kazi hiyo ya usafi wa mazingira kuanza
rasmi kwa maadhimisho ya sherehe za kutimia Miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar
ya Mwaka 1964 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
alikabidhi zawadi ya vifaa tofauti vya usafi wa mazingira kwa Kikundi cha
usafi wa Mazingira cha Kilimani { Kilimani City }.
0 comments:
Post a Comment