December 02, 2015

Bodi ya mapato Zanzibar ZRB imeifunga ofisi ya kampuni ya simu ya VODACOM kwa kushindwa kulipa kodi kuanzia Disemba 2014 hadi Juni 2015.
Afisa uhusiano wa bodi hiyo Makame Khamis Mohamed amesema kamupini hiyo ilipaswa kuwasilisha marejesho yao na malipo chini ya 30 Novemba lakini hawakufanya hivyo wakati taarifa wamepelekea  hadi kwa maandishi.
Amesema Vodacom kama kampuni nyengine zilizopo Zanzibar wanawajibika kulipa kodi kwa mujibu wa sheria ya kodi namba 7 ya 2009 na sheria 4 ya kodi ya ongezeko la thamani ya 1998.
Makame amefahamisha kuwa kutokana na hali hiyo ZRB imelazimika kuchukua uamuzi huo kutokana na vodacom kushindwa kuwasilisha marejesho yao bila ya taarifa yeyote
Nae mwakilishi wa Vodacom upande wa Zanzibar Mohamed Mansour amesema suala hilo liko nje ya uwezo wao kwa kuwa kuna miingiliano ya usimamizi wa kodi kati ya serikali ya Tanzania na ya Zanzibar.
Amefahamisha kuwa kutokana na hali hiyo kampuni hiyo imekuwa ikilipa moja kwa moja mamlaka ya mapato Tanzania TRA  hivyo ni vizuri ZRB  kudai huko.

Hata hivyo Mansour amesema kwa sasa wanafanya juhudi za kufanya mazungumzo na tra kutatua tatizo hilo linalo wakwamisha kuanya kazi kwa ufanisi.   


0 comments:

Post a Comment