December 03, 2015


Waziri mkuu, Kassim Majaliwa amefanya tena ziara ya kushtukiza bandari ya Dar es Salaam na Shirika la reli Tanzania TRL na kubaini upotevu wa makontena zaidi ya 2431.
Akiwa bandarini hapo amekagua mfumo wa utoaji na uingizaji mizigo akiwa na ripoti ya ukaguzi inayoonyesha majina ya waliopitisha makontena hayo bila kulipiwa kodi.
Katika maongezi ya awali alihakikishiwa kuwa mfumo hauruhusu kontena kuibiwa lakini waziri mkuu aligundua hali hiyo.
Kufuatia hali hiyo ametoa muda wa masaa matatu hadi saa kumi na mbili jioni leo apewe tarifa dhidi ya hatua zilizochukuliwa kwa wahusika.
Alipotembelea shirika la reli waziri mkuu majaliwa amegundua mabilioni ya fedha zimetumika na miradi iliyokusudiwa bado haijatekelezwa.

0 comments:

Post a Comment