December 03, 2015


Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt.John  Pombe  Magufuli ametoa siku  saba kwa wafanyabiashara walioingiza mizigo kwa kukwepa kodi kulipa mara moja kodi kwani watachukuliwa hatua kali za kisheria.
Ametoa agizo hilo leo Ikulu  jijini Dar es Salaam alipokuwa na mkutano na wadau wa sekta binafsi kuwasikiliza maoni  yao ikiwa ni sehemu ya ahadi zake katika kipindi cha kampeni za kuomba kura za kiti cha Urais,lengo likiwa ni kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta binafsi.
Amesema ni lazima wadau hao kuweka maslahi ya taifa mbele ili kuweza kujenga taifa lenye maendeleo makubwa ya kiuchumi.
Rais Magufuli ameendelea kusema kuwa katika kipindi hichi cha miaka mitano amedhamiria kuijenga nchi na watu wasimuelewe vibaya kwa maamuzi anayofanya kwani ni kwania njema ya kuleta maendeleo.
Pamoja na hayo Mheshimiwa Dkt.Magufuli ameaahidi kutoa ushirikiano kwa wadau wa sekta binafsi hasa wazalendo  kwa vile wanamchango mkubwa katika kukuza uchumi.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) Regnald Mengi amemuomba  Rais Magufuli kuendelea kukemea masuala ya rushwa  pamoja kusaidia kupunguza utitiri wa kodi Tanzania.


0 comments:

Post a Comment