December 08, 2015


Klabu ya Waandishi wa habari kisiwani Pemba, Pemba Press Club -PPC imelaani kitendo cha kuchomwa moto kwa kituo cha Radio cha Hist FM kilichopo Migombani Mjini Unguja hivi karibuni.

Kituo hicho kilichomwa moto desemba 2 majira ya  7:30 baada ya watu  zaidi ya 15 kukivamia wakiwa na silaha huku wamejifunika nyuso na kusabisha hasara inayokadiriwa kuwa ni zaidi ya shilingi milioni 70.
Katibu wa klabu hiyo Khatib Juma Mjaja amesema wanahabari wa Pemba, hawafurahishwi na vitendo vyovyote vya kuhujumu au vinavyokwaza uhuru wa habari kwa namna yoyote ile kwani haki ya habari ni miongoni mwa haki muhimu zinatambuliwa na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 na katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Amesema kitendo hicho kimelenga kukwamisha demokrasia ya habari kwa jamii ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
PPC imeziomba taasisi zinazohusika kulifanyia kazi suala hilo na sheria kuchukuwa mkono wake kwa wote watakaobainika mkuhusika na kitendo hicho dhalimu.
“kile ni kitendo cha kinyama na kinapaswa kulaniwa na kila mtu, kinasikitisha sana na kimeweza kurudisha nyuma maisha ya watu, watu wanategemea kuendesha familia zao pale halafu wanakwamishwa na watu wachache”amesema.
Amesema tasnia ya habari imekuwa kihimiza maendeleo ya nchi, ikiwemo vijana kujiajiri wenyewe na kutokutegemea ajira kutoka serekalini, amevitaka vilabu vya habari kuwa mtari wa mbele kukisaidia kituo hicho kwa hali namali.

0 comments:

Post a Comment