December 13, 2015


Waalimu Nchini wametakiwa kuwapa fursa na kuwahamasisha wanafunzi kushiriki katika michezo  ili kuwezesha  kupata timu nzuri na kushiriki katika mashindano ya Kimataifa.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari Utamaduni Wasanii na Michezo Tanzania Leona Tadeo   alipokua akifunga Shamrashamra za  Tamasha siku ya Walimu Duniani katika  Uwanja wa Amani mjini zanzibar.
Amesema nchini Tanzania wananchi wengi wanalamika kwa kutofanya vizuri katika michezo  kutokana na  kukosekana vijana waliojengeka kimichezo tangu wadogo jambo linalorejesha nyuma  maendeleo ya michezo hiyo.
Amesema jukumu hilo kuwajenga wanafunzi kimichezo linapaswa kutekelezwa na waalimu wakati wapo watoto wakiwa skulini.
Kwa upande wake mwalimu Mussa  Abdulrabi  kutoka Wizara ya Elimu amesema lengo la tamasha hilo ni walimu kushiriki michezo mbalimbali ili kuonesha vipaji vyao  katika michezo hiyo.
Sambamba na hayo mwalimu huyo ameaahidi kuwa watawashajiisha walimu wenzao kwenda kujiunga na Chuo cha Maendeleo   ya Michezo ili  kupata walimu wengi  ili kuungana nia ya Serekali katika kuendeleza Michezo .
Katika shamrashamra hizo kumefanyika michezo ya kuvuta kamba, Mpira wa Mkono, mbio za Gunia pamoja na Mpira wa miguu  iliyowshirikisha walimu kutoka Mkoa Kusini Unguja, Mkoa wa mjini Magharib na Mkoa wa Kaskazini.






Maelezo Zanzibar
   

0 comments:

Post a Comment