December 13, 2015


Mufti mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zuberi, amewakosoa baadhi ya masheikh walioshindwa kuwajibika na kusema watu kama hao wanawatia aibu waislamu. 
Akizungumza mjini dar es salaam  amewataka viongozi wa Baraza kuu la waislamu Tanzania BAKWATA  kubadili fikra na mienendo yao katika utendaji ili iwe dira kwa waislamu. 
Amesema bakwata ina sura mpya na malengo makuu ni kuwaunganisha waislamu, na kusisitiza kuwa, umoja waumini hao utasaidia kuwa na nafasi muhimu katika masuala  ya kitaifa.
Mufti mkuu ameongeza pia BAKWATA itaanzisha kitengo cha masuala ya uchumi kitakachoongozwa na wataalamu watakaokuwa na jukumu la kuiandaa jamii ya kiislamu kushiriki kukuza uchumi wa nchi. 
Mufti zuberi ameanza ziara ya kuzunguka nchi nzima kuhamasisha umoja na mshikamano miongoni mwa waislamu. 

0 comments:

Post a Comment