Uongozi
wa Mkoa wa Kusini Unguja umetoa muda wa wiki mbili kwa hoteli ya Palumbo reef
Beach Resort ya Uroa kuondoa
mawe waliyoyaweka katika maeneo ya ufukwe iliyopo karibu na hoteli hiyo.
Pia umekataza pia uchotaji mchanga
katika maeneo ya fukwe za bahari za kigaeni Makunduchi na ukataji wa miti ya
mikoko katika eneo la Bwejuu banja.
Mkuu
wa mkoa huo Dkt Idrissa Muslim Hijja amesema vitendo hivyo vinahatarisha
kupotea rasilimali hizo zisizorejesheka pamoja na kupoteza haiba ya maeneo ya
fukwe ambayo ni moja ya kivutio kwa utalii wa Zanzibar
Akitoa
agizo la kwa hoteli ya Palumboreef
Beach Resort amesema mawe hayo yameziba njia na kusababishia kero
kubwa kwa wanakijiji cha uroa kupita njia hiyo wanayoitumia kufanya shughuli
zao mbali mbali za kijamii ikiwemo ya uvuvi na ukulimaji mwani.
Dkt
Idrissa amefahamisha kuwa hoteli hiyo
imekiuka taratibu za sheria kutokana na
muwekazaji huyo kutokuwa na kibali chochote
kinachomruhusu kuziba njia hiyo jambo linaloweza kusababisha uharibifu
wa mazingira katika maeneo hayo ya fukwe za bahari.
Aidha amesisitiza kwa wawekezaji kuacha kujichukulia maamuzi yao kinyume na taratibu za zilizowekwa na serikali na badala yake ni vyema kufuata sheria pamoja
na kujenga uhusiano mzuri na wanavijiji
ili kuondokana na migogoro isiyo ya lazima.
Nae Mkuu wa wilaya ya kusini unguja Khamis Jabir
Makame akizungumzia marufuku ya uchotaji wa mchanga katika maeneo ya fukwe za
bahari na ukataji wa miti ya
mikoko amesema serikali
haitomvumilia mwananchi yoyote atakayebainika kuhusika na vitendo hivyo
kwani vinaleta athari kubwa za uharibifu
wa mazingira.
ameliagiza
jeshi la polisi kwa kushirikiana na maofisa mazingira na misitu kuhakikisha
wanalishughulikia ipasavyo suala hilo ili kukomesha vitendo hivyo.
Afisa
mazingira wilayani humo Ramadhani Haji Ameri amesema pamoja na hatua zinazochukuliwa za kuelimisha
wananchi kuhusu utunzaji wa mazingira baharini bado wanapuuza suala hilo na
kuendeleza kwa kasi vitendo hivyohali inayorudisha nyuma juhudi za serikali
katika kulinda rasilimali za taifa.
0 comments:
Post a Comment