December 14, 2015



Waziri wa habari, Utamaduni, sanaa na michezo Nape Moses Nnauye amewatoa hofu wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini hususani Magazeti pamoja na wanahabari kuwa atahakikisha anakuwa mlezi wa vyombo vya habari pamoja waandishi wa habari ili vifanye kazi kwa  umakini.
Akizungumza na watumishi na wakuu wa taasisi za wizara hiyo jijini Dar es salaam mara baada ya kuwasili katika afisi za wizara hiyo Nape amesema kuteuliwa nafasi hiyo isiwatie hofu  kuwa atautaathiri muhimili huo wa habari.
Amesema ufinyu wa bajeti ni miongoni mwa  changamoto zinazoikabili wizara hiyo hivyo amesema atahakikisha anaibana serikali ili kuongeza bajeti kwa wizara hiyo kwa lengo la kutekeleza majukumu yake vizuri.


 
Naibu waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Anastazia James Wambura (kushoto) akimkaribisha waziri wa wizara hiyo
katika ofisi za wizara hiyo leo jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa naMichezoMhe.Nape Moses Nnauye
akiongea na waandishi wa Habari katika ofisi za wizara hiyo kwa mara
ya kwanza tangu ateuliwe kuwaWaziri. Mhe Nape amehaidi kuleta
maendeleo kupitia wizara hiyo kwa hali na mali.

0 comments:

Post a Comment