December 09, 2015


UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi UVCCM umesema unaunga mkono kasi ya utekelezaji kazi wa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Magufuli na kinachofanyika sasa ndio chachu ya maendeleo ya Watanzania.
Umesema utaendelea kumuunga mkono katika kila hatua kwa lengo la kuona vijana wote wa Tanzania wanarudi katika ari ya uwajibikaji kama ilivyokuwa wakati wa serikali ya awamu ya kwanza.
Aidha, umesema kinachofanywa sasa ni  ni kutekeleza kwa vitendo sera za CCM zilizoainoshwa katika ilani yake ya uchaguzi ya mwaka 2015/2020 .
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka amesema hayo  mara baada ya kumaliza kazi ya usafishaji  mazingira katika maadhimisho ya miaka 54  ya uhuru wa Tanganyika  mara baada ya kuongoza usafi huo  katika eneo la la Kigogo,jijini  Dar es Salaam.
Amesema Dk. Magufuli katika mikutano yake yote ya kampeni wakati akiomba kura kwa wananchi, aliahidi kuongozwa na sera za Chama, malengo na mikakati itakayoleta maendeleo ya kweli.
 Amesema kuwa Mafanikio hayo na kasi ya Dkt. Magufuli  ya utendaji kamwe haiwezi kutenganishwa na ubora wa sera zilizomo katika ilani ya uchaguzi ya CCM.
 Kwa mujibu wa Shaka, UVCCM itaendelea kumuunga mkono kwa vitendo Dk. Magufuli katika malengo ya serikali yake hasa kupiga vita rushwa, maonevu, ubadhirifu wa mali za umma, mkakati wa udhibiti na matumizi bora ya rasilimali na maliasil za Taifa na kuhimiza uwajibikaji maeneo ya uzalishaji mali.
 Kuhusu kasi ya  serikali katika kuwachukulia hatua watendaji wazembe, kuwaweka kando wale  wenye  tuhuma za ufujaji na  wizi wa fedha za serikali, shaka amefafanua  wakati wa kuoneana muhali au kubebana umekwisha na sasa ni kazi kwenda mbele.
Katika kuunga mkono agizo la Rais Magufuli  kaimu katibu mkuu huyo amemesahuri makatibu wote wa mikoa na wilaya kulifanya zoezi hilo kuwa endelevu na kila juma mosi ya mwisho wa  mwezi kuwa siku ya usafi utakakuwa ukisimamiwa na Vijana wote nchini. 

0 comments:

Post a Comment