December 31, 2015

Katibu mkuu afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar Dadi Shajak amesema uchumi wa Zanzibar pekee hauwezi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Amesema ili kutekeleza maazimio yaliyofikiwa katika mkutano wa kimataifa wa hali ya hewa uliofanyika mjini Paris Ufaransa hivi karibuni Zanzibar inahitaji  kuungwa mkono  na jumuiya na mashirika ya kimataifa ili kukabiliana na hali hiyo.
Akizungumza katika mkutano na kamati ya uongozi ya mabadiliko ya tabia nchi Dkt shajak amesema tayari Zanzibar  ina maeneo 147 yaliyoathirika hivyo kuna haja ya kuunga mkono maazimio yaliyofikiwa katika mkutano huo.
Nae Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya usimamizi wa mazingira Zanzibar Sheha Mjaja Juma miundo mbinu mingi inaweza kupotea na kuharibika kwa iwapo juhudi za makusudi hazitachukuliwa na wadau wa mazingira.
Amesema kinachopaswa ni kuandaliwa program mbali mbali za kuhimili mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni pamaoja na kutoa elimu kwa jamii na uwezo wa kifedha teknologia.

Kwa upande wake Afisa mazingira kutoka ofisi wa Makamu wa kwanza wa Rais Soud Mohamed Juma amewataka wananchi kupunguza vitendo vya kukata miti ovyo na kuharibu rasilimali kwa kiwango kikubwa.

0 comments:

Post a Comment