Mamlaka ya kuzuia rushwa
na uhujumu uchumi Zanzibar imebaini kuwepo mianya ya rushwa inayotumika katika baadhi
ya taasisi za umma za serikali.
Kutokana na hali hiyo
imejaribu kutoa ushauri wa kuimarisha mifumo ya utendaji wa taasisi hizo
ikiwemo Idara ya usafiri na Leseni, Halmashauri ya wilaya ya Magharibi na Idara
ya vizazi na vifo ili kuondosha vitendo vya ubadhirifu katika utoaji wa huduma
kwa wananchi.
Hayo yamebainishwa katika
taarifa ya taasisi hiyo kwa vyombo vya habari kuhusu maadhimisho ya siku ya
mapambano ya kuzia rushwa duniani yenye kauli mbiu “Kata minyororo ya rushwa” imefanikiwa
kupokea malalamiko 125, sitini na sita kati yao yamefanyiwa uchunguzi na
10 yamefikishwa afisi ya mkurugenzi wa mashtaka ili kuchukuliwa
hatua za kisheria.
Katika malalamiko hayo pia
tuhuma 45 zimefutwa kutokana na kutokuwa na ushahidi wa kutosha dhidi ya
vitendo hivyo.
Taarifa hiyo ilotiwa saini
na Mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Mussa Haji Ali imeeleza kuwa bado tatizo la rushwa ni kubwa na inadumaza
maendeleo ya jamii na taifa huku taasisi hiyo ikikabiliwa na changamoto kadhaa
katika mapambano yake Zanzibar.
Moja ya changamoto iliyotajwa
ni ushiriki wa mdogo wa jamii kutokana na uelewa wao mdogo juu ya athari za
rushwa huku wakiwa na matumani ya kupata mabadiliko makubwa ya kulimaliza hasa tatizo
hilo baada ya kuanzishwa taasisi hiyo.
Mkurugenzi huyo wa Mamlaka
ya kuzuia rushwa na uhujumu uchumi Zanzibar ameeleza kuwa wameandaa mpango
makakati wa miaka mitano wa maadili ya kuzuia rushwa utakao sisitiza wajibu wa
taasisi za serikali ili kufanikisha vita
dhidi ya tatizo hilo nchini.
0 comments:
Post a Comment