December 12, 2015


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein ameizinuda meli mpya ya MV Mapinduzi II iliyonunliwa na Serikali bandarini mjini Zanzibar.
Meli  hiyo  imetengenezwa na kampuni ya Daewoo nchini Korea ya  kusini imewasili Zanzibar wiki iliyopita ya Disemba 2, 2015 imegharimu  dola  za kimarekani milioni 30.6 ina  uwezo wa kuchukua abiria 1200 tani 200 za mizigo.
Akizingumza katika uzinduzi huo Rais Shein amesema serikali imeamua kuinunua meli hiyo ili kuipunguzia majanga yanayoikumba Zanzibar kutokana na kuwepo  meli chakavu zilizokuwa ziwahudumia wananchi.
Amesema MV Mapinduzi II ni bora na mpya na hakuna ulaghai wa kuidanganya serikali ulifanyika wa kuiuzia meli iliyokuwa imeshatumika.  
“Wananchi Msisikilize maneno ya mitaani kuwa hii Meli imeshatumika suala hilo halina ukweli,”. Amesema Dkt Shein.
Amefahamisha kuwa serikali kwa sasa imeamua kuimarisha sekta ya usafiri wa baharini kwa kulifanyia mageuzi Shirika la meli ili lifanye kazi ya biashara yenye tija kwa vile ni sekta hiyo ndiyo nyenzo muhimu ya kuongeza  pato  la taifa.
Dkt Shein ameongeza kuwa kwa sasa Serikali inategemea kuanza ujenzi Bandari kubwa ya mizigo eneo la Maruhubi mpiga duri na tayari imeshaanza makubaliano na Serikali ya China kuanza ujenzi huo kuanzia mwaka ujao ikiwa ni juhudi za kuimarisha sekta ya usafirishaji wa baharini.






0 comments:

Post a Comment