December 02, 2015


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dr Ali Mohmaed Shein Serikali imepania kuhahakisha sheria zinafuatwa na imekusudia kuchukuwa hatua kali kwa wanaozikiuka.
Amesema katika miaka mitano iliyopita sheria nyingi na kali zimepitishwa kama vile za uhujumu uchumi na sheria ya maadili ya viongozi.
Hivyo Dk Shein amewataka wafanyabishara na viongozi wenye dhamana kuzitekeleza ipasavyo na si suala la kuelezewa kila mara.
Alikuwa akijibu namna Serikali inavyo chukuwa hatua katika kuendana na kasi ya kupambana na maovu katika jamii hasa ufisadi katika ziara fupi ya kutembelea eneo litakalojengwa bandari mpya ya Mpigaduri.
Rais shein ameeleza kuwa mradi huo unaotarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwaka 2016 pamoja na ule wa upanuzi wa kiwanja cha ndege cha Abeid Amani Karume ni hatua muhimu ya kuongeza kasi ya kukua uchumi na kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii Zanzibar.
Ujenzi wa bandari mpya ya Mpigaduri utakuwa wa awamu tatu ambapo awamu ya kwanza ya ujenzi huo utagharimu Dola za kimarekani milioni 231.4 itaanza mwezi Januari, 2016 na itajengwa na Kampuni ya CHEC kutoka nchini China.
Huu ni mradi mkubwa kwa uchumi wetu hivyo wananchi watarajie maendeleo makubwa na yenye kasi zaidi ya uchumi wetu” Dk. Shein alieleza.
Amewaambia waandishi wa habari na viongozi waliokuwepo kuwa mradi huo wa ujenzi wa bandari ya Mpigaduri si mradi mpya ulianza tangu Awamu iliyoongozwa na Dk. Salmin Amour na  awamu hii ndio umefanikiwa kufikia hatua ya utekelezaji.
Sisi awamu hii tumekwenda mbele zaidi,tumetafuta fedha na tumefanikiwa kutokana na urafiki wetu na serikali ya Jamhuri ya Watu wa China tutapata mkopo wa kujenga bandari hii” Dk. Shein alidokeza.



0 comments:

Post a Comment