Chama cha Mapinduzi CCM
Zanzibar kimewataka wanachama
wake kujiweka tayari na kujitokeza kwa wingi katika Uchaguzi wa marudio
mara tarehe itakapotangazwa.
Wakati CCM ikitoa kauli
hiyo Chama cha Wananchi CUF Zanzibar kimesema hakipo tayari kupokea maazimio ya
mazungumzo ya kutafuta mwafaka wa Uchaguzi Mkuu kama yatakuwa yanakwenda
kinyume na maamuzi waliofanya wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 Mwaka
huu uliofutwa.
Kauli
ya ccm imetolewa katika taarifa kwa waandihsi wa habari kuhusu kuhusu
kikao cha siku moja cha kamati maalum ya NEC Zanzibar kilichofanyika afisi kuu ya ccm Kisiwandui mjini Unguja iliyosainiwa na Katibu wa Kamati
Maalum ya itikadi na Uenezi Waride Bakari Jabu.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo imewataka wafuasi wake kujitayarisha ili kukiletea
ushindi wa kishindo Chama Cha Mapinduzi Zanzibar kuanzia Rais, Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi na Madiwani wakati utakapowadia.
Taarifa
hiyo imeeleza kuwa Kikao hicho kilichofanyika leo Jumapili kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Dkt.
Ali Mohamed Shein ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi kimeridhia pia majadiliano yanayoendelea kuhusu hali ya Kisiasa
Zanzibar yanayoshirikisha Viongozi kadhaa.
Viongozi
hao ni pamoja na Marais Wastaafu wa Zanzibar Ali Hassan Mwinyi, Mhe, Dkt.
Salmin Amour Juma na Amani Abeid Karume, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Iddi.
Aidha
kimempongeza Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kushinda katika Uchaguzi
Mkuu wa Oktoba 25, 2015 na Samia Suluhu Hassan, kuwa Makamu wa Tanzania.
0 comments:
Post a Comment