Wananchi wanaoishi karibu na eneo lililotengwa kwa ajili ya
ujenzi wa Hospitali ya Rufaa katika kijiji cha Binguni, Wilaya ya Kati Unguja wameanza kulivamia eneo hilo kwa shughuli za ujenzi wa nyumba za kuishi.
Eneo hilo la ekari 80 Wizara ya Afya linakusudiwa kujengwa
Hospitali hiyo kubwa pamoja na nyumba za wafanyakazi.
Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Dkt. Idrissa Islam Hija amesema
wananchi wamekuwa watukutu kufuata sheria za nchi na kila wanalofanya ni haki
yao licha ya hatua za kuwaelimisha na kuwazuilia kuchukuliwa.
Amesema hayo katika ziara ya kuliangalia eneo hilo la wizara
ya afya iliyofanywa na uongozi wa Wizara ya Afya ukiongozwa na Naibu Waziri wa
Wizara hiyo Mahmoud Thabit Kombo.
Mkuu wa Mkoa amesema eneo hilo limepimwa rasmi na Serikali kwa
ajili ya matumzi ya Wizara hiyo hivyo matumizi mengine yeyote yatakayofanywa
hayatatambuliwa na uongozi wa Mkoa.
Amewataka wananchi wanaoishi karibu kutolitumia kwa shughuli
yeyote ya ujenzi ili kujiepusha na hasara inayoweza kuwapata baadae.
Dkt. Idrissa Islam Hija ameishauri Wizara ya Afya kuanza
hatua ya kulizungushia uzio ili wananchi wasipate mwanya wa kulivamia.
Aidha amewataka masheha na madiwani wa eneo la Binguni kutotowa
vibali vinavyowaruhusu wananchi kujenga kwani uzoefu unaonyesha watu
wanaovamizi maeneo kwa kujenga nyumba hupatiwa vibali na masheha ama
madiwani.
“Madiwani na Masheha hamuruhusiki kutoa vibali vya
matumizi ya ardhi na kufanya hivyo ni kosa jiepusheni na tabia hiyo hasa
katika eneo hili lilitengwa kwa ajili ya shughuli za Serikali,” amesisitiza
Mkuu wa Mkoa.
Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo ameuagiza uongozi
wa Wilaya ya Kati na Mkoa wa Kusini Unguja kuwazuiya wananchi wawili walioanza
ujenzi katika eneo hilo na kuwataka kuvunja nyumba hizo
haraka iwezekanavyo.
Amesema iwapo watashindwa kuvunja majengo hayo wenyewe
Wizara itasimamia kuvunja nyumba hizo na watalalipia gharama zote.
Maelezo Zanzibar
0 comments:
Post a Comment