December 04, 2015


Jeshi la Polisi Nchini limeelezea faraja yake kutokana na mfumo wa Viongozi wa Kitaifa kuonyesha muelekeo wa kuwajali watumishi wao kutoka Taasisi tofauti za Umma na hata binafsi hasa wale watumishi wa ngazi ya chini.
Afisa wa Polisi S.P Zakaria Benard ameeleza hayo alipokuwa akitoa shukrani za Jeshi hilo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliyefika katika Kata ya Goba Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es salaam kutoa mkono wa pole na kuifariji Familia ya Koplo Yesaya Mwakambi aliyefariki Dunia kwa ajali ya Piki pili Ubungo Jijini Dar es salaam.
Koplo Yesaya ni miongoni mwa Askari wa Usalama Bara barani wa Jeshi la Polisi Nchini wanaowajibika kuiongoza Misafara ya Viongozi Wakuu wa Kitaifa akiwemo  wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alipata ajali akiwa kazini mwezi Mmoja na nusu uliopita .
Kamanda Zakaria amempongeza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kwa uamuzi wake wa kutenga muda kwa lengo la kuifariji Familia ya Koplo Yesaya.
Akitoa shukrani kwa niaba ya wanafamilia wa Koplo huyo Mchungaji Isaya Isaleka ameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuisadia Familia ya Marehemu Koplo Yesaya Mwakambi ili iweze kuwa na nguvu za kukabiliana na maisha yao ya baadaye.
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akiifariji familia hiyo inayoongozwa na Mke wa Marehemu  Bibi Wema Sanga amewataka   kwa kuwa na moyo wa subira  hasa Mkewe Mama wa watoto wawili Bibi Wema Sanga kwa kuondokewa na mpendwa wao.
Afisa wa Polisi S.P Zakaria Benard akitoa shukrani kwa niaba ya Jeshi la Polisi kwa uamuzi wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif  wa kuifariji familia ya askari wa ngazi ya chini ya Jeshi la Polisi Nchini Marehemu Yesaya aliyefariki kwa ajali ya Piki piki akiwa kazini.


Mke wa Marehemu Koplo Yesaya Bibi Wema Sanya wa kwanza kutoka kulia akiwa na Dada yake pamoja na watoto wake wawili wakati wakipewa mkono wa pole na  Balozi Seif aliyefika kwenye Kata yao ya  Goba Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es salaam kuwafariji baada ya kufiwa na mpendwa wao.






Othman  Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
4/12/215.

0 comments:

Post a Comment