December 01, 2015



Mradi mkubwa wa Kimataifa wa ujenzi wa kisiwa cha Kitalii   kitatengezezwa kwa mfumo wa ufukiaji Bahari umeanza rasmi katika eneo la Hoteli ya Utalii iliyopo Mtoni Marine kaskazini Magharibi ya Mji wa Zanzibar.
Hata hivyo gharama kamili za Mradi huo bado hazijafahamika  hadi utakapokamilika  rasmi ujenzi wake hapo baadaye.
Mradi huo unaoendeshwa na Kampuni ya Kizalendo  ya Bakhresa Group utahusisha ujenzi wa Hoteli ya Kimataifa ya Ghorofa  Tano ya Daraja la Tano  (Five Star+), eneo la wazi la mapumziko pamoja na kutengeneza  Kisiwa cha Mji mpya .
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kampuni hiyo Said Salim Bakhresa amesema ujenzi wa mradi huo ni muhimu kwa uchumi na  utasaidia mapato ya Taifa pamoja na kutoa ajira kubwa kwa vijana wazalendo.
Nae Mhandisi wa Mradi huo Ahmed Shamsi amesema ujazaji wa mchanga katika eneo linalofukiwa unafanyika kwa kutumia chombo maalum chenye uwezo wa kunyonya  na kusafirisha mchanga kutoka ndani ya Bahari na kukata Majabali.
 Amefahamisha kuwa kazi ya uchimbaji na kufukia mchanga katika eneo hilo zilianza Mwezi uliopita wa Novemba zinatarajiwa kukamilika mwezi ujao wa January.
Akitoa nasaha zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipitembelea kuangalia kazi hiyo amemupongeza Uongozi wa Bakhresa Group kwa uamuzi wa kuanzisha mradi huo mkubwa uliozoeleka katika Mataifa yaliyoendelea ambao utakapo kamilika utasaidia kuitangaza Zanzibar na Tanzania kiutalii Kimataifa.
Mfumo huo wa ufukiaji Bahari kwa ajili ya kuanzisha miradi ya Kiuchumi ni mfumo unaotumiwa na Mataifa mbali mbali Duniani na kwa Afrika  mradi kama huo umeshafanyika katika Kisiwa cha Seycheles.
Chombo maalum kinachotumika kwa kazi ya uchimbaji wa mchanga Baharini  Chenye  uwezo wa kunyonya  na kusafirisha mchanga kutoka ndani ya Bahari sambamba na kukata Majabali na kufukia katika eneo linalotengenezwa kisiwa cha Mji Mpya mtoni Marine.
Sehemu  inayoendelea kufukiwa hapo Mtoni Marine ambayo itatumika hapo baadaye kwa ajili ya eneo maalum litakalotoa fursa kwa Wananchi  kupata mapumziko .
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif wa Pili kutoka Kulia akiwa  na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baghresa Group Bwana Said Salim Baghresa wakishuhudia harakati za kunyonya  na kusafirisha mchanga kutoka ndani ya Bahari kwa chombo maalum hapo Mtoni Marine




Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamui wa Pili wa Rais wa Zanzibar
1/12/2015.
  

0 comments:

Post a Comment