November 17, 2015


Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) inakusudia kuanzisha mfumo wa kulipa kodi  kwa njia  ya mtandao “oline payment” ili kuwaondolea usumbufu wafanyabiashara.
Afisa uhusiano wa bodi hiyo Makame Khamis Mohamed amesema lengo ni kuhakikisha inatoa huduma bora kwa walipa kodi ili kuwasilisha mauzo yao kwa njia za kisasa Zanzibar.
“Endapo tukifanikiwa hatua hii ya huduma ya kulipia kwa mtandao basi ZRB tutachukua jukumu la kuwajuilisha wafanyabiashara wetu ili kuanza kutumia mfumo huo mara moja.
Afisa mohamed amesema mbali na kuondoa usumbufu pia njia hiyo ya mtandao italeta ufanisi katika ukusanyaji wa kodi pamoja na kuwasilisha mrejesho kwa walipa kodi.
Hata hivyo amewaomba wafanyabiashara wote kuendelea kutumia huduma ziliopo sasa huku  ZRB ikiwa katika harakati za kuhakikisha inaendelea kuboresha huduma hizo.
Hadi Machi mwaka 2015 ZRB Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) ilikusanya mapato ya kodi ya Sh. bilioni 135.7 sawa na asilimia  95 ya makadirio ya miezi tisa hadi kufikia mwezi huo.

0 comments:

Post a Comment