Madiwani walioteuliwa ni 1393 kutoka katika Vyama vya CCM, CHADEMA, NCCR- MAGEUZI
pamoja na CUF huku 15 wakisubiri chaguzi ZA
kata 34 zimalizike katika kata zilizosalia ili kufikisha idadi ya madiwani 1402
wa kuteuliwa.
Akizungumza na
waandishi wa habari Mkurugenzi wa
Uchaguzi Ramadhani Kailima Amesema katika madiwani hao walioteuliwa alifafanua
CCM 1,021, Chadema 280, CUF 79, ACT- Wazalendo 6 na NCCR Mageuzi 6.
Amesema
halmshauri ambazo bado hazijakamilisha uchaguzi zitasubiri uchaguzi ukamilike
kwa kata zote ndiyo waunde baraza la halmashauri na kazi ya kwanza kwa baraza
hilo ni kuchagua meya wa halmashauri husika.
Mkurugenzi huyo
wa Uchaguzi NEC amesema kuwa ni Desemba 20 mwaka huu, ndio tarehe
ya mwisho wa Uchaguzi katika Majimbo na Kata zilizokuwa hazikufanya Uchaguzi .
0 comments:
Post a Comment